RIWAYA JINI HUSNAT
MTUNZI: ZUBERI MAVUGO
SEHEMU YA PILI
ilipofika jioni wakati anajiandaa kuondoka ghafla mlango ukafunguliwa na HUSNAT akaingia na tabasamu pana usoni uzuri wake ulikuwa mara mbili ya mwanzo bumbuwazi likauvaa uso wa VERGA akutegemea kama angekuja kweli mbona secretary wake ajampgia simu? alijawa na khofu ulochanganyikana na woga ilikuwa lazima aogope alikuwa kavaa gauni jekundu refu lililo mkaa vyema.akaenda kuketi kwenye viti vya wageni na kumpa mkono VERGA........
Mbona SECRETARY wake MOURENE ajampigia simu kumwambia juu ya mtu kumuitaji? au akumwona? au amemdhuru? au naye ameogopa? maswali hayo mfululizo yakakishambulia kichwa chake! akakiri kutoyajua majibu yake akagutuka baada ya kuuona mkono wa JINI yule
"vipi sweet?" sauti tamu imtoaye nyoka pangoni ilipenya katikati ya ngoma ya masikio yake ikawa burudani tosha ndani ya mfumo mzima wa masikio! lakin burudani hiyo katu aikuwepo katika ubongo wake ubongo wake ulikuwa katika tafakari zito tafakari lililomezwa na woga.JOHN VERGAN alitaitika! alikuwa akitetemeka na kusogea nyuma mara ghafla kiti kikadondoka!
"unaogopa nini sweet au aunipendi?" HUSNA kwa mara nyingine tena akauliza! VERGAN akujibu! akabaki kimya
"VERGA TAMBUA NA KUPENDA! NA UKIKUBALI KUWA NA MIMI NITAKUTAJIRISHA UTAMILIKI MALI NYINGI ZAIDI YA HIZI!,MAVIWANDA,MAKAMPUNI,UTATEMBEA DUNIA NZIMA UNAVYOTAKA UTAPOKEA ZABUNI MPAKA MWENYEWE UTAZIRINGIA LAKINI UKINI KATAA NTAKUFILISI UTARUDI KIJIJINI MASIKINI MTAOMBA HADI VYAKULA NA UTAISHI MAISHA YA MATESO KATIKA DUNIA HII UTAKUWA UKIZARAULIWA NA KILA MTU CHAGUA MOJA.....KUMBUKA USINIKATAE KISA MIMI NI JINI! TAMBUA HATA SISI MAJINI TUNA MIOYO YA KUPENDA KWA DHATI ZAIDI YENU NYINYI BINADAMU HIVYO MOYO WANGU UPO KWAKO WEWE VERGA AU UJAVUTIWA NA MIMI?" aliuliza HUSNA huku akiwa anatembea tembea ofisini mule
"hapana! hapan...." ghafla kitasa cha mlangoni kikawa kina tingishika kuonesha mlango unafunguliwa kutoka nje "JINI HUSNAT AKATOWEKA apo apo"
"bosi unaongea na nani? bosi kuna nini? bosi mbona chini umefanya nini?" MOURINE alimuuliza maswali Mfululizo VERGA aliyekuwa kadondokea kwenye pembe ya nyumba
"ulivyo ingia ujamwona mtu?"
"mtu? mtu gani bosi mbona sikuelewi?"
"HUSNA! ujamwona HUSNAT?"
"Husna ndo nani bosi?"
kabla VERGAN ajajibu swali lile HUSNA akatokea na kumnyooshea VERGAN kidole mdomoni ishara ya kunyamaza.
"amna kitu MOURINE kaendelee na kazI"
"Amna kitu MOURINE kaendelee na kazi!"
alijibu VERGAN huku akinyanyuka na kujifuta futa vumbi HUSNAT ALISHATOWEKA!
"Bosi kuna wale watu wa idara ya mapato wanasema watakuja kesho ivyo uandae risiti zote"
"sa...w ni.meku..elewa" VERGAN alijibu kwa kubabaika secretary wake akaondoka VERGA akarud kwenye kiti chake na kukaa kitu "AKIKUKALIKA!" alinyanyuka na kuchukua koti! lake la suti lililokuwa nyuma ya kiti chake na kulivaa.akachukua simu na kumpigia MOURINE
"Namuitaji ZUBER"
"Sawa bosi"
baada ya muda ZUBER akaingia,
"sasa wewe kijana kaa hapa ofisini mimi naenda kupumzika kidogo"
"sawa bosi"
JOHN VERGAN akachukua brufcase yake na kuondoka!,aliitaji kupumzika aliisi kichwa kinamuuma,katu akujua balaa alilokuwa akilifata mbele yake
ZUBER alitafuta ma file na kuendelea kuyajaza taratibu! akujua kinachoendelea yeye alikuwa na yake kichwani katika kudhihirisha ule usemi umdhaniaye ndiye kumbe siye,au rafik yako ndiyo hadui yako,ZUBER alikuwa ni chui kwenye ngozi ya VERGAN ama kweli usilo lijua ni sawa na usiku wa kiza.
na kwa upande wa MOURINE secretary wa VERGAN kiti akikukalika! alijua bosi wake ana matatizo tu! japo hakuwai kumwambia kuwa anampenda ila moyoni mwake alikiri kumpenda sana bosi wake yule! hapa kuna kitu na lazima nifanye kitu kumsaidia bosi wangu wakati akiwa anawaza hayo ghafla arufu kali ya manukato ikaanza kusikika,upepo mkali ukaanza kuvuma! vumbi lililotengeneza kimbunga cha wastani kikaanza kuingia ndani na kupeperusha ma file yale pale mezani,makabati yakaanza kujifunga na kujifungua yenyewe na mara mtoto mzuri mrefu alovaa nguo ndefu akatokea! katikat ya chumba kile MOURINE akataka kukimbia akashindwa,akataka kupiga kelele pia akashindwa akabaki na butwaa "mimi naitwa "ZAIDATU BINT ROUJAT" ukoo wa kifalme wa kijini nimekuja kwa ajili ya msaada kwako.ila lazima ufe" kabla MOURINE ajafanya kitu JINI ZAIDATU akamvamia na kumnyonya damu yake.
******
JINI ZAIDATU baada ya kuakikisha amemuangamiza secretary yule MOURINE kwa kumfonza damu yake yote akaa chia ukelele mkubwa! kisha akatoweka! mara ghafla MOURINE akazinduka ilikuwa kama kazinduka toka usingizini! ila MOURINE huyu alikuwa tofauti na wa mwanzo! macho yake yalingaa! meno yalichongoka mawili! ila ghafla vyote vikatoweka akabaki MOURINE wa mwanzo! ZAIDATU alikuwa kaingia katika mwili wa MOURINE kwa kazi maalumu! ni kazi gani? aliijua moyoni mwake.aliendelea kufanya kazi zake kama kawaida.machoni alionekana ni MOURINE ila kumbe alikuwa ni jini hatari ilikuwa ni PATASHIKA.
Moyoni mwa ZUBER wazo lililotawala kichwa chake ni kuakikisha mali zote za VERGAN zinakuwa chini yake kwa namna gani? ilo alikumsumbua akakwa pua simu ilokuwa pale mezani na kupiga namba kadhaa akaweka mkonga wa simu yake maskioni "MOURINE nakwomba uniunganishe na PITER"
"sawa bosi" MOURINE aliitikia.na kuwaunganisha wakaongea machache.
dakika chache zilizofatia PITER au mwanasheria mkuu wa compuny ile alikuw mbele ya bosi wake yule. "nachotaka kuongea na wewe ni siri kukiwa na makubaliano au hata kama kusipokuwa na makubaliano!" ZUBERI alifungua kikao kile kwa onyo kali.
"na kama siri hii ikivuja sitokuwa na kingine zaidi ya kukuua!"
"what?" PITER aliamaki
"ndiyo! ni dili litakalo badilisha maisha yetu tutakuwa matajiri wakubwa kama bosi VERGA"
"SAWA nipo tayari weka kazi mezani!" PITER Alikubaliana na wazo la ZUBER na kuwa tayari kusikia dili lenyewe
"naitaji tutaifishe compuny hii iwe chini yetu! mimi na faida tugawane amsini kwa hamsini"
"unasema?"
"ndiyo naitaji compuny hii iwe chini yetu"
"sijakuelewa ZUBER ni vipi tutafanikisha ili?"
"swali zuri PITER wewe ni mwanasheria wa compuny una nyaraka hati zote muhimu ni kitendo cha kuzibadilisha tu"
"tatizo itakuwa nisahii yake"
"atatekwa na kulazimishwa kuweka sahii baada ya hapo tutamuua"
"sawa ZUBER nimekuelewa niachie nianze kazi..
*******
JOHN VERGAN alifika nyumbani kwake na mlinzi akafungua geti VERGAN akaingiza gari taratibu.mlinzi alimsalimia lakini VERGAN akuitikia.kichwa kilikuwa kikiwaka moto akaenda mpaka chumbani kwake na kujitupa mara ghafla akapitiwa na usingizi wakati akiwa yupo usingizini akaota yupo na JINI HUSNA akiwa pembezoni mwa jabali palipokuwa pameota majabali makubwa wakiwa wameegemeana kimapenzi HUSNA akasema:
"dear nna zawadi yako!"
"zawad gan sweet?" VERGAN akaoji akiwa kaushika mkono wa dada yule mrembo
"funga macho yako"
VERGAN akafumba HUSNA akatoa mkufu wa dhahabu na kumvalisha VERGA
"Fungua!"
VERGAN alipofumbua macho yake akuamini akamkumbatia kwa nguvu HUSNA mkufu ule ulikuwa ukimeremeta huku ukiandika jina la VERGAN ulikuwa na picha ya HUSNA na VERGAN wakiwa wamekumbatiana.Baada ya VERGAN kumkumbatia akamwachia ghafla akashangaa kumuona kabadilika kawa na sura mbaya ya kutisha meno yalochongoka pembe pembeni ya vichwa kucha ndefu VERGA akashindwa kuvumilia na kupiga kelele ghafla akazinduka.
"he! kumbe ilikuwa ni ndoto?"
VERGAN alitahayari alishindwa kuzuia mshangao dhahiri katika macho yake.wakati akiwa anashangaa wakati akiwa bado kakaa kitako kitandani.alipocheki pembeni ya kitanda AKAUONA ULE MKUFU! aliruka kitandani na kutaka kukimbia MLANGO UKAJIFUNGA kizaa zaa kikaanza.kelele za msichana akicheka zikasikika.
"VERGAN kwa nini unielewi? kwa nini utaki kunipenda? kwa nini utaki kunizoea? ama uitaji kuwa nami? niambie VERGAN nijue,hata mimi na moyo VERGAN!" ilisikika sauti ikisema na kimya kikafuata mlango ghafla ukafunguka.VERGAN kama mweu akatoka mbio alikimbia hadi getini mlinzi wake ndiye aliyefanikiwa kumzuia
"bosi wangu utaumia! una matatizo gani bosi tell me why?"
"niache! niache! niache KITALU niache!" (come down bosi come down punguza presha,relax,smile ,then tell me why ili niweze kukupa msaada) twende ukaone mkufu twende jini si ndoto ni kweli! VERGAN aliropoka.
***************
VERGAN na mlinzi wake KITALU waliongozana hadi ndani VERGA akiwa na lengo la kumuonesha ule mkufu wa ajabu! mkufu wa ndotoni walipofika AWAKUKUTA KITU!,MKUFU AUKUWEPO,VERGAN akakunguta mashuka lakini bado mkufu aukuonekana.ikabidi kwa maneno kuntu,maneno ya hisia VERGA amsimulie mgambo wake yule!
"bosi wangu! jambo doncho sana ili!,ili ni jini mahaba na kuna ustadh! swadakta maalim! sheghe ni shidaaaa! hana uwezo wa kumwita! kumpumbaza! kumkamata na kumfinyanga hadi aitwe marehemu anaitwa maalim sheghe RAJAB!"
"unaweza kunipeleka saivi kwa maalim?"
"bila shaka kabosi kangu! lakini pale kagetini katakaa kanani?"
"uc of pale ntamtafuta mtu mwingine"
"akah! na mimi si ntakosa ka kazi bos?!"
"hapana we ntakupandisha cheo utaenda katika compuny yang na ela itapanda."
"sawa bosi ngoja nkajiandae ili tukaka angamize ako kajini mahaba!"
ile saa KITALU anageuka tu nyuma akakumbana na mkono dhabiti! mkono imara wa HUSNA! lakin VERGAN akumwona KITALU alihisi kukabwa ghafla akaanza kukooa damu alikuwa akionesha kidole shingoni alipokabwa mara akadondoka chini na kufa hapo hapo.HUSNA akiwa na uso wa hasira akaiangalia kwa chuki maiti ile akairuka na kuweka mikono juu akatoweka.VERGA alichanganyikiwa! kitalu hakuwa mzima na sasa ni marehemu! kivipi? bado lilikuwa swali lisilo na jibu
polisi walikuja na kumchukua VERGA na house garl wake JASMIN na mwili wa marehemu ukapelekwa hospitalini kwa uchunguzi zaidi.alama za mikono shingoni zilionekana dhahiri! hivyo madaktari wakaanza kudili nazo.
cha ajabu alama za mikononi za JOHN VERGAN ndo zilizo onekana shingoni mwa MLINZI MACHACHARI KITALU.mshatakiwa namba moja akawa JOHN akawekwa chini ya ulinzi! moyo ulimuuma maswali ya siyo na majibu yakatiririka kichwani kwake.familia yake baba mama zote walikuja kumtembelea wakamtoa khofu kwa kuweka mawakili hatari pesa si ilikwepo.tarehe ya kuanza kusikilizwa kwa kesi ikafika.baada ya kuamishwa katika mahaka
****************
SERIKALI ikapandisha shaidi namba moja! ambaye alitambulika kama afande MARWA.
MWENDESHA MASHTAKA@"taja majina yako matatu"
SHAIDI NO 1@ "MARWA JAFETY JOHN"
MW/MASHTAK@ "Unaweza kutuambia kilichotokea siku ya tukio?"
SHAID NO 1 "Yap nilikuwa kituoni siku hiyo mara simu ikaita kupokea ni msichana aliyekuwa akilia alidai bosi wake alikuwa akimnyonga mlinzi wake ndipo nilipochukua afande wengine mpaka eneo la tukio tulipofika tulimkuta mtuhumiwa kashafanya mauaji ndo tukawaweka yeye na house garl chin ya ulinzi"
maelezo haya ya AFANDE marwa yalimshtua kila mtu akiwepo JOHN VERGAN ambaye yeye ndiyo aliyepiga simu polisi iweje aambiwe ni mfanyakazi wake? pia mawakili wake walitazamana kwa kutoamini wakisikiacho kesi kwa upande wao ilizidi kuwa ngumu na kwa upande wa house gar yule alishangaa kuambiwa eti alipiga simu wakati bosi wake ndo alipiga ilikuwaje? kuna nin? ilikuwa ni mkanganyiko katika mioyo yao katu awakujua kuwa:
wakati JOHN VERGAN anapiga simu kituoni sauti yake iliishia mule ndani lakin katika masikio ya afande MARWA ilisikika sauti ya binti akiongea kwa jazba,woga,huyu si mwingine ni JINI HUSNAT aliyeyameza maneno ya VERGAN na kuongea kama JASMIN.ndivyo ilivyokuwa.
MW/MASHTAKA "mshtakiwa una swali lolote kwa shaidi no 1"
VERGAN "ndyo mh! afande marwa mimi ndo nlikupigia simu iweje useme ni JASMINI kwa nini lakin inakuwa hivi?"
baada ya kuuliza swali VERGAN akaanza kulaumu ikabidi akatishwe na nafas kurudi upande wa mawakili
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni